Hutofutika moyoni
Hutonitoka rohoni
Utabakia maishani
Taabuni na furahani
Umeiweka alama
Itabaki imesimama
Moyoni imezama
Haiwezi kunihama
Mimi nilipofikia
Siwezi kujisifia
Ni wewe nakusifia
Na Muumba yarabia
Sikuoni machoni
Sikusikii masikioni
Nakuona taswirani
Nakuwaza akilini
Wewe ni tunu yangu
Ewe mzazi wangu
Nitakukumbuka mama yangu
Siku za maisha yangu!
Kwa rafiki yangu mpendwa anayekumbuka miaka sita leo toka mama mpendwa atangulie mbele ya haki.
Tupo pamoja kaka.
ReplyDeleteNi kweli hakuna kama mama
Tumwombee kwa sala.Amina
Pole Mkuu!
ReplyDeleteNimatumaini yangu katika kumbukumbu huumii tu lakini,...
.... kwa kuwa naamini MAMA angependa uendeleze libeneke kwa furaha kwa baraka zake pia!
Ni wazo langu tu kwa sauti Mkuu!