20/04/2009

Deci Yazikwa Rasmi

Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam jana, alipokuwa akitoa tamko la msimamo wa serikali kuhusu shughuli zilizokuwa zinaendeshwa na Kampuni ya Deci (Tanzania) Limited.

SIKU chache baada ya kusimamishwa shughuli za Taasisi ya Development Enterpreneurship Community Initiative (Deci), serikali imetangaza kufunga akaunti zote za wamiliki wake na kudhibiti maeneo yote ya shughuli za taasisi hiyo kwa lengo la kuwezesha kurudisha fedha kwa wananchi.

Tamko hilo la Serikali limetolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo katika mkutano na waaandishi wa habari makao makuu ya wizara hiyo huku waziri huyo akiwaweka waandishi ukumbi wa mikutano kwa zaidi ya saa moja na nusu kumsubiri.

Kauli hiyo ya Serikali imekuja wakati wanachama wa taasisi hiyo wakiwa katika hali tata kutojua hatima ya mbegu zao walizopanda wakati wakisubiri hatima ya uchunguzi wa serikali.

Waziri Mkulo aliyeelezwa kuanza mkutano saa sita na robo, mchana aliingia ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo saa 7. 48 na kueleza kuwa " Tamko nitakalolitoa ni zito na muhimu, limepitiwa na kukubaliwa na Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais. Mimi natoa tamko la serikali kama waziri kwa ababu shughuli za taasisi hiyo zinaihusu wizara yangu ya Fedha na uchumi:

"Ilibidi wakubwa walipitie na kuidhinisha, ni tamko linalojitosheleza kwa kila hali, lina kurasa 21, lakini hapa nimefupisha hadi kufikia kurasa tatu,"alisema Mkulo.

Alisema Deci imeamua kusitisha shughuli zake hatua ambayo imesababisha wasiwasi mwingi miongoni mwa wanachama wake na kwamba serikali imeamua "Kuhakikisha maeneo yote ya shughuli za Deci yanadhibitiwa, kukinga pesa zote zilizopo katika akaunti za waendeshaji wa Deci na Deci yenyewe hadi hatma ya shughuli za Deci itakapojulikana."

Waziri Mkulo alibainisha kuwa "Serikali inaendelea na hatua za kuhakikisha waendeshaji na wamiliki wote wa Deci hawatoroki."

Kwa undani zaidi bofya hapa

Wadau Mnasemaje juu ya hatua hii ya serikali?

9 comments:

  1. Hodi kibarazani nimepita kusalimia nimekuona kwa dada Koero.

    ReplyDelete
  2. Karibu Dada Yasinta,
    Karibu bila kusita
    Furaha mgeni kupata
    Kwangu baraka kuweka

    Kwako huwa naingia
    Maisha barazania
    Link nimekuwekea
    Waweza ona kulia

    Tuendeleze libeneke
    Ukweli uelezeke
    Nia zetu tuziweke
    Nchi tuiezeke!

    ReplyDelete
  3. Nami nimekuona kwa Da Koero nikaona nijiunge kukukaribisha. Asante kwa kuwa nasi na kutuweka kwenye list ya magazeti tando. Nami nitafanya hivyo kwangu na nitashiriki mijadala endelevu iliyopo hapa kwa kadri ya uwezo wangu.
    Karibu na KARIBU SANA

    ReplyDelete
  4. Ahsante sana mzee wa changamoto!
    Tupo pamoja na jiko na moto!

    ReplyDelete
  5. Sijui nimepotea njia......
    Hivi niko wapi hapa............Duh!!!!1
    Aaaahh!!!!! Sijapotea.......
    haya mwenye mji huu upoooo!!!!!!
    Nimepita hapa namtafuta kuku wangu sijui nimemkuta?
    habari za siku kaka, mzee wa sosholojia,
    nilikuwa na pilika pilika za hapa na pale lakini leo alfajiri nimepita hapa kukusalimia nikielekea shamba.
    haya nikirudi nitapita kukujulia hali......
    Karibu tena VUKANI.....

    ReplyDelete
  6. Dada Koero hujapotea,hapa ni kwangu nyumbani
    Jiwe niliegemezea, nikaingia chumbani
    Sautiyo ikipenyea, hodi hodi humu ndani
    Karibu dada Koero, kuku wako nilimuona

    Kuku wako nilimuona, akila mchangani
    Kwa kuwa anajulikana, hapa kwangu nyumbani
    Rangi zake nzuri sana,anashika usukani
    Karibu dada Koero, kuku wako nilimuona

    Nashukuru umeahidi, kunipitia ukirudi
    Unibebee na mahindi, VUKANI unaporudi
    Nami nakuahidi, kwako nitabisha hodi
    Karibu dada Koero, kuku wako nilimuona

    ReplyDelete
  7. Haya nimerudi Shamba na kwa bahati mbaya sijakukuta, ila nimemkuta mwanao, kijimzigo chako cha mahindi nimeegemeza hapo upenuni, kuku wangu nitamfuata kesho nimeambiwa na mwanao kuwa anatamia.
    Mwaka huu naona mvua za vuli zimechelewa....sijuia ndio ule mwaka wa njaa ushaanza?......haya ukila ukumbuke kuweka akiba

    ReplyDelete
  8. Dada Koero ahsante sana, kijimzigo nimekipata
    Kidogo tu tumepishana, mwanangu kanifuata
    Nilikwenda kumuona, Mzee Masulupweta
    Nimekuta analia sana, huku moyo wampwita

    Anasema hana amani, kapoteza fedha zake
    Amepanda mbegu shambani, kabana mifuko yake
    Amekuta miba shambani, katika mipaka yake
    Masulupweta analia sana, huku moyo wampwita

    Mimi nikamfariji, ajikaze kisabuni
    Hata nikampa uji, pale kwake upenuni
    Asikimbilie jiji,kule serikalini
    Masulupweta analia sana, huku moyo wampwita

    Wakati nikimliwaza, mwanangu alinijia
    Ndipo akaninong'oneza, mgeni katupitia
    Upepo nikaukimbiza, nyumbani kufikia
    Dada Koero nashukuru sana, kijimzigo nimekipata

    ReplyDelete
  9. Mfikishie pole zake huyo Mzee Masulupwete,
    Mwambie asikate tamaa, kwani kila baya nyuma yake kuna zuri limefichama....

    ReplyDelete