03/05/2013

Utenzi wa Da' Gloria



Gloria D. Gonsalves

Jamani Nampenda


Jamani nampenda,
kaka yule wa kisambaa,
lakini hanielewi,
ninapotamka mahaba.
Wee mndele una nini,
hata honga hujui,
na dumange lako kutu,
mie namkunda Makibua.
Sikukata tamaa kamwe,
nikajaribu bahati yangu,
kaka naitangwa Mamtoi,
natokea Korogwe.
Kughamba kishambaa huteia,
Kiimo na kudika pia shida,
niache nikagoshe,
huko kwako seniuye.
Jamani nampenda,
kaka huyu Shekalaghe,
laiti Mzee Shauri angalikuwepo,
angenisaidia kumzindika.

Translation:
Dear me, how I love him,
that Sambaa man,
but he understands not,
when I speak of love.
Woman what have you,
you can’t hello in Kisambaa,
and you lack mdumange skills,
I had rather love Makibua.
I did not give up,
and tried my luck in his dialect,
my name is Mamtoi,
I come from Korogwe.
You are unable to speak Kisambaa,
neither can you farm nor cook,
let me go to sleep,
and shall not return to yours.
Dear me, how I love him,
this man named Shekalaghe,
if late Shauri was alive,
he would help me charm him.

*Other translations: Kisambaa (language of Sambaa tribe found in Usambara mountains of Tanzania), mdumange (traditional dance of the Sambaa people), Shauri (a Sambaa man R.I.P, who popularized mdumange dance in the media and was a traditional healer)*

18/04/2013

Kutoka "Mjengoni":Yaliyokusanywa na Mwanazuoni


Yameandikwa mengi kuhusu hali ya ukosefu wa staha na heshima na matumizi ya maneno ya kukera inayoendelea kwa baadhi ya wabunge katika vikao vinavyoendelea bungeni ("Mjengoni") Dodoma. Mwanazuoni Machunde Mauma amejaribu kupitia vyanzo mbalimbali vya habari na kukusanya hatimaye kuorodhesha baadhi ya nukuu ya maneno ya kukera  zinazotumiwa na baadhi ya wabunge hao....

1. ‘‘Kuna wabunge ambao wana mimba sizizotarajiwa bungeni...”
-Mbunge wa Mtera (CCM),Livingstone Lusinde
  
2. "Sugu naomba unyamaze. Mimi ndiye nazungumza. Mimi siongei na mbwa,naongea na 
mwenye mbwa"
-Mbunge wa Kondoa Kusini (CCM),Juma Nkamia

3.“UDOM (Chuo Kikuu cha Dodoma) kuna udini wa hali ya juu, wanafunzi wa dini tofauti hawalali chumba kimoja.”
-Mbunge wa Rombo (CHADEMA),Joseph Selasini

4."Kwa kuwa wanaume wengi wanabaka, kifunguliwe kituo wafundishwe kutongoza.”
-Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Leticia Nyerere

5.“Serikali iruhusu raia wa Tanzania walime bangi wapate fedha za kigeni.”
-Mbunge wa Nkasi (CCM), Ally Kesi

6.‘‘Mambo mengi nchi hii hayaendi kutokana na serikali pumbavu, hatuwezi kuwa na waziri wa elimu boya...”
-Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA), Joseph Mbilinyi

7. "Siwezi kuikubali taarifa hiyo. Nadhani huyu mtu bado amechanganyikiwa na uchaguzi wa kenya. Mimi sijaitaja Chadema bali nimesema kuna chama kimoja cha siasa, SIJUI YEYE ANAWASHWA NINI..!!
-Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde

8. "Serikali ina tatizo kwa kuwa kuna akili ndogo inatawala vichwa vikubwa.”
-Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA),Mchungaji Peter Msingwa

9. "Mbowe kaja hapa anajambajamba tu" ..."Wewe Msigwa ni mchungaji wa watu au mchungaji wa nguruwe?
-Mbunge wa Konde (CUF), Khatibu Saidi Haji

10. "Wanaume wanapoongea,watoto wa kiume wakae chini"
-Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM) Mwigulu Nchemba



Kama hali hii imefikia hapa kwa mhimili huu muhimu wa dola ni dhahiri kuwa tunakoelekea si kwema asilani! 

17/04/2013

Kurejea Rasmi!


Ni takribani miezi mitano sasa imepita tokea kubandikwa kwa "bandiko" la mwisho katika kibaraza chetu hiki. Tena "bandiko" lenyewe liliwekwa baada ya "ka-muda" fulani kupita! Hii yote ilitokana na sababu ambazo hazikuweza kuepukika, zilizopelekea kukosekana kabisa hata "ka-upenyo" kubandika chochote.

Kipindi chote hiki hakika kilikuwa kinarindima sambamba na hamu ya kurejea rasmi kibarazani. Hamu hii ikitangulizwa na nia na mikakati ya kuboresha zaidi kibaraza chetu, kuhakikisha kuwa pamoja na mambo mengine, kutokosekana kabisa kwa "mabandiko".

Kwa maneno hayo machache kwa sasa, Mwenyekiti anatangaza kurejea rasmi kwa kibaraza chetu.

28/11/2012

New Book-A Must Read!


 Newly published book by Mwanazuoni Fatima Bapumia. Currently you can purchase this book through Amazon and other online bookstores.

19/06/2012

18/06/2012

Hongera Dkt. Thomas Joseph Ndaluka!

Dkt. Thomas Joseph Ndaluka akitetea tasnifu yake ya shahada ya uzamivu


  
Dkt. Thomas Joseph Ndaluka a.k.a Tojo, mhadhiri wa Sosholojia kutoka idara ya Sosholojia na Anthropolojia ya Chuo Kikuu Dar es Salaam, kampasi ya Mwalimu J.K Nyerere (zamani Mlimani), amekula nondozzz yake ya shahada ya uzamivu (PhD) baada ya kutetea vyema tasnifu yake Religious Discourse, Social Cohesion and Conflict: Muslim-Christian Relations in Tanzania katika chuo cha Radboud, the Netherlands. Kibaraza hiki kinachukua nafasi hii kutoa pongezi za dhati kwa Dkt. Thomas Joseph Ndaluka kwa hatua hii. 

Wanajopo, katikati aliyevaa suti na tai ni Dkt. Abu Mvungi, mmoja wa wasimamizi wa Dkt Thomas

Jiandae pia kupata chapisho lake jipya la kitabu juu ya dini, migogoro, mshikamano na mahusiano ya kati ya waislamu na wakristo Tanzania kwa kubofya HAPA

16/06/2012

Mom you loved us!


Today has marked the third year since you passed away mom, Magreth Mabula-Senga.
Mom you loved us from our first breath, 
held our hands through the years, 
guided us along the paths that our lives took, taught us that there is nothing we can't make it through to hold our faith and follow our hearts. You gave us your all and asked nothing in return.

We will always love you mom,
We will carry you with us each day in our hearts. 
We will mourn our loss but rejoice that you are in a better place sitting with your loved ones, awaiting our arrival one day.




09/06/2012

"Hepi Besdei" kwa Dommy na Pinu!

Dominick "Dommy" akiwa na "braza" wake Agripinus "Pinu"
Leo tarehe 9 Juni ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Dominick Mathew Senga a.k.a Dommy na kesho tarehe 10 Juni ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Agripinus Mathew Senga a.k.a Pinu. Dommy na Pinu ni uzao wa kiume wa Mwanasosholojia. Kibaraza hiki kinawatakia kumbukumbu njema na baraka tele Dommy na Pinu. Kibaraza kinawaambia kwa king'eng'e...
 
May the cup of your life be full of sweets and savories, hopes and dreams, success and accolades. Happy Birthday dear sons


16/05/2012

Waraka wa Maige "Fesibuku"


Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Ezekiel Maige ameandika waraka ufuatao na kuupachika katika ukurasa wake wa Facebook.

Ndugu zangu na rafiki zangu. Kwanza niwape pole kwa mshituko mlioupata kwa haya yaliyojitokeza. Naomba msisikitike sana. Kila jambo alilopanga Mola hutokea kadiri ya mapenzi yake. Route ya maisha ya mwanadamu hupangwa na Mola mara tu anapompulizia pumzi ya uhai. Hili lilipangwa hata kabla sijatokea duniani miaka 42 iliyopita!

Mungu hakushindwa kumwokoa mwanawe Yesu asisulubiwe, tena kwa kuonewa! Hasha, tungeupataje ukombozi bila hilo kutokea? Wakati mwingine Mungu hutoa nafasi kwa mambomagumu kuwafika waja wake, si kwamba hawapendi,bali ili unabii utimie. Ilifika wakati hata Yesu akaona kama Mungu kamuacha! Hasa sisi kwa hili tunaweza kudhani Mungu katuacha! Hasha, ni njia ya kuufikia ukombozi wa kweli.


Pili, kwa kifupi sana, niwafahamishe kuwa, yaliyotokea ni ushahidi kwamba maliasili ni ngumu. Kukabiliala na wabaya ni kazi ngumu. Wapo waliojipanga ukiwavamia ovyoovyo unaondoka wewe. Ndivyo ilivyotokea.


Niwahakikishie, wazalendo wamepoteza mpambanaji. Nimepambana na wahalifu angani, majini, porini, mijini na vijijini ndani na nje ya nchi. Nilitumia kila aina ya uwezo wangu kulizawadia taifa langu utumishi uliotukuka. Sikubakisha chembe ya energy.


Waziri gani aliyesimamia sheria na kuwapa vitalu watanzania maskini wenye sifa na kuwaacha wazungu kama sheria ilivyoelekeza?


Waziri gani aliyewafikisha mahakamni watorosha twiga akina Kamrani na wenzake? Watu wametumia records za matukio ya 2009/10 kuficha matendo na maamuzi ya kishujaa ya maige ya 2011. Yawezekana hawakutaka nipate sifa, lakini ipo siku nitaipata. Tena si siku nyingi. Niliwaomba wenzangu wamwogope Mungu. Bado nasisisitza hivyo, si Mungu wangu kama ilivyodhaniwa, bali Mungu wetu wa haki.


Waziri gani aliyefunga biashara ya wanyamahai?


Waziri gani aliyeonyesha mfano wa kuchukua hatua kwa watumishi pale alipoona hawatendi sawa? Maige hakusita kuchukua hatua.


Maamuzi haya ni magumu na yamegusa watu wenye nguvu na ushawishi mkubwa. Nilitegemea vita hii, na ninaamini tutashinda. Nilisema Bungeni, watanzania wapenda haki wanisikilize kwa makini. Muda haukuruhusu, ila nitarudi Bungeni na nitasema.


Imesemwa issue ya nyumba. Nimefafanua na kutoa vielelezo. Kila mbunge aliyetaka amekopeshwa shs 290m, wengine wameanzisha biashara na wengine wamenununua magari na wengine majumba. Wapo walioficha, na tupo tuliojiweka wazi! Mkopo wangu huo umekuwa my contribution na balance kulipwa na benki na nyumba kuimortgage. Nimetoa nyaraka zote kwa wanahabari na vyombo vyote husika. Nimesema mwenye mashaka aende kwa Msajili wa hati wizara ya ardhi, au kwa kamishna wa maadili, au CRDB Azikiwe na Dodoma nilikokopa au amtafute muuzaji. Kote huko utapata rekodi ya bei na mode of payment. Wapo wahuni, kwa maslahi ya kisiasa na chuki binafsi wametangaza bei tofauti na niliyonunulia. Manasheria wangu anashughulikia hilo.


Niwahakikishie, vita nimepigana, imani na dhamana nimeilinda, muda wa kutuzwa na mwenye kumbukumbu sahihi, Mungu utafika. Naamini nimejiwekea akiba isyooza Mbiguni.


Yapo mengi yasiyo sahihi yaliyosemwa. Nitakuwa nafafanua kila nipatapo fursa na muda utazidi kutufunua. Kwa kifupi, kwa suala la vitalu, hakuna kampuni hata moja iliyopewa kitalu cha uwindaji bila kuomba, kukaguliwa na kamati ya ushauri na hatimaye kupewa alama. Kampuni zisizokuwa na sifa ni zile zilizopata chini ya alama 50. Na kwa kampuni zilizokuwa kwenye biashara, passmark ni alama 40 kwa mujibu wa kanuni ya 16(5) ya kanuni za uwindaji wa kitalii za mwaka 2010. Hakuna kampuni iliyopata chini ya alama 50 iliyopata kitalu. Hakuna kampuni ya kizalendo iliyopendekezwa na kamati ya ushauri ambayo haikupewa kitalu.


Kwa upande wa report ya CAG, haikunigusa binafsi kwani ilikuwa inaishia juni 2010 wakati mimi ilishika dhamana Novemba 2010.


Kwa upande wa biashara ya wanyamahai, hakuna wanyama waliosafirishwa kinyume cha sheria wakati wangu (2011), na matukio ya utoroshaji tulipoyabaini, tulifungua mashitaka kwa watuhumiwa nakufnug biashara hiyo.


Naanza kazi ya kuwawakilisha wananchi wa Msalala. Nitawawakilisha kwa mujibu wa katiba na ahadi zangu kwao hadi 2015 watakapopata fursa ya kuamua vinginevyo.


Mara nyingi watenda mema hufanyiwa hiyana. Kwa wakristo, naomba msome Mwanzo 4:1-15.


Wasalaam.

14/05/2012

Tafakuri ya Mbumbumbu





Na Emmanuely Deodath
 
Siwachukii CCM kwa sababu ya rangi za vitenge vyao na kamwe sintowapenda CHADEMA
kwa sababu ya magwanda yao ya khaki!

Kidumu Chama Cha Mapinduziiiiii…..! japo sijaweza kujua hiki chama ni cha mapinduzi yepi!
Kweli chama kikadumu…kimedumu kwa muda sasa! mpaka juzi juzi kilipoanza kudumaa. Chama
hakikudumu kwa mda wote huu eti kwa sababu mwenyikiti alisema chama kidumu nasi kuitika
kidumuuuuu….. kilidumu kwa sababu mwanzoni kilijengwa katika misingi ya mambo
yaliyodumu.
Halafu enzi hizo naona kama walikuwa hawavai sana vitenge vya kijani..au inawezekana
walikuwa wakivivaa ila tatizo ni picha zilikuwa za “black and white”, anyways….hoja si walivaa
nini, la hasha…hoja ni kwamba walifanya nini na kwa nani..unaona eeh! Chama chini ya
Mwalimu kilikataa kuburuzwa na Mabwanyeye, mabwanyenye wa ndani na wa nje, chama
kikataa viongozi kujilimbikizia mali na wakatekeleza kwa vitendo! Mfanyakazi wa umma
aliruhusiwa kulipwa kwa kazi moja tu! Hiyo ya pili na ya tatu zilikuwa ni za kujitolea kwa ajili ya
ujenzi wa taifa. Vipi leo? Mambo yakoje….na ndo maana nakichukia hiki chama, dili zinapigwa
kuanzia kwa mkuu wa kaya mpaka kwa wanazuoni….
Chama kilimilikishwa kwa wakulima na wafanyakazi, wafanyabiasiasa hawakuawa na nafasi.
Akina mzee Kaduma wanatuambia ulikuwa ukiitwa na Mwalimu unajipanga kisawasawa! Kwa
sababu Mwalimu hakuwa na mzaha ati! leo hii Doctor akikuita unaweza hata ukamvungia tu!
Hana noma…Kwa nini lakini? Doctor si mkubwa kuliko Mwalimu, au? Anyways huu ndiyo
uliokuwa mfumo wa uongozi, hakukuwa na utawala….leo hii hakuna uongozi kuna bora utawala
bora…..
Sasa wamekuja jamaa wa pipoooozzz..pawaaaa! hawa jamaa sijui wanasema chama ni mali ya
nani? Sijawahi kujua walau…wamejijenga katika misingi gani… Kwa mtizamo wangu wamejenga
chama katika hasira za wakulima na wafanyakazi dhidi ya CHICHIEM! Mimi huwa nikiwaonaga
hawa jamaa na yale magwanda yao huwa napagawa naona kama nimemwona Cheguavara!
Nasema hata waweke JIWE na CHICHIEM waweke mgombea mtu..ntalipigia JIWE LA
KHAKI…Lakini najiuliza, tayari katika mfumo wa uongozi wa chama na uwakilishi, ndani ya
CHADEMA kuna MAJIWE mangapi?? Nini mtizamo na mipango yao ya baadae endapo CCM
itapotea katika ramani na hatutakuwa na wakumchukia tena?? Au wanampango wa kuwa
wapinzani milele?? Ndani ya chama hiki nani tumtumainie…? Maana dah! Au ni Yule mzee Baba
paroko wa zamani asiye na hisa katika hii kampuni….sorry chama? Mapenzi yangu kwa hiki
chama si mapenzi ya upofu..ni mapenzi yanayoona..yanapoona kizuri yanapongeza na kibaya
kinapotokea nakemeaaa! Tusiwe na hasira kiasi cha kuchagua MAWE..walau basi ukilichagua lioombee lipate upako ligeuke kuwa MTU! Sijui kama umenisoma??? Japokuwa kwa sasa ni
ukweli ulio wazi kuwa CHADEMA ndiyo mbadala pekee wa CHICHIEM.

07/04/2012

Which April, Kanumba?‏

Steven Kanumba

By Erick Kabendera
 
The news of Steve Kanumba’s sudden death seemed like a fictitious scene from a horror movie; you see a character dying but your instincts remind you that it’s just a movie and that the actor is still alive in actual life.
Unfortunately, the case of Kanumba is different; he is dead. And such a bitter truth may take a long time for the family and fans of the actor to come to terms with the fact that the young man who worked so hard to achieve success in his acting career had his life cut short before his full potential could be realized.
I rarely interact with local actors. But last month I found myself in the company of Mr. Kanumba, arguably this country’s most charming actor. As the news of his untimely death reached me today, it made me remember a scene which led to that first encounter with him a few weeks.
His childhood friend, Bongo Flava artist Haji Nurah told him a journalist wanted to see him, and he agreed, and chose our meeting to take place at Sinza Vatican one chilly Friday evening.
Upon arriving there, we drove through a small path and finally parked in front of a moderately luxurious house where three cars, a Lexus and two others, were parked.
“They are all Kanumba’s,” Nurah slowly whispered.
We were invited into the living room, which was neatly decorated with silver ornaments and white painted walls and well placed curtains with a comfortable sofa set. The elegant space gave an impression one sees reflected in the perfectionism that characterised his movies, his fans tell me.
After waiting for ten minutes, a young man emerged from a room in shorts and a sleeveless T-shirt. His face bared a sad smile and he seemed slightly unsettled.
The night before, he had had a slight car accident and a fight with his girlfriend. He chose not reveal who the lady was.
 
To read more, click HERE

06/04/2012

Barua ya wazi kwa Joshua Nassari

Mbunge Mteule wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari



BARUA YA WAZI KWA Ndg. JOSHUA NASSARI, MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI
Ndugu Joshua,

Natumai umepata pongezi za kutosha juu ya kushinda kwako katika kinyang’anyiro cha Ubunge. Ushindi wako haukua lelemama. Nchi nzima iligeuzia macho na masikio yake Arumeru. Uliposhinda ndipo nilipogundua kuwa hukuwa chaguo la Wanaarumeru wala wapenzi wa Chadema. Kila niliyekutana naye alilitaja jina lako kwa furaha huku akishangilia kushindwa kwa CCM. Hapa Chuoni (UDSM), ushindi wako ulikuwa gumzo. Mtaani umejaa vinywani mwa watu. Kwa utafiti mdogo nilioufanya, wengi wamefurahia zaidi kuporomoka kwa ngome ya CCM.

Kwa ukubwa wa majukumu uliyopewa na matumaini uliyotwishwa, nadhani hata wewe unatishikatishika. Binafsi nachelea kukupongeza. Kila nikutazamapo naona nyuso za vikongwe, akina mama na wototo wenye njaa, waliodhoofu na wagonjwa. Nawaona vijana wasio na ajira na waliokata tama. Naona umbali mrefu watembeao akinamama kuteka maji. Nawaona yatima, wajane, n.k. Nawaona wanafunzi waliofukuzwa shule na vyuo kwa kukosa ada… Wamepoteza matumaini, wote wanakutazama wewe kama jibu la matatizo yao. Huo ni upande mmoja. Upande wa pili, naona watu wakipanga kugawana fedha za kodi na miradi ya maendeleo. Naona jinsi rasilimali za nchi hii zinavyoneemesha mataifa ya nje na vijibwa vyao vya hapa nchini. Na wewe upo katikati ukipiga makelele, kama kilivyo chama chako [kiitikadi?]. Je, ni silaha gani  utakazotumia kurejesha matumaini kwa wanyonge?

Tafakuri ilinipeleka mbali na kunifanya nikumbuke Januari 2009, nikiwa mwasisi wa Bunge Kivuli la Vijana wa Dar es Salaam (DSM Youth Shadow Parliament – DAYOSHPA). Hili lilikuwa jukwaa la aina yake ambalo liliwakutanisha vijana wa makundi mbalimbali ili kujadili namna ya kuboresha mfumo wa elimu hapa nchini. Hii ilikuwa ni baada ya mgomo mkubwa wa wanafunzi wa vyuo vikuu wakipinga mfumo wa madaraja ya mikopo uliopelekea kufungwa kwa vyuo vikuu vya umma takribani nane. Jukwaa hili halikuwa na mfadhili. Lilikuwa ni jukwaa la vijana na liliondeshwa kwa nguvu ya vijana bila kulipwa chochote.

Kuna mmoja wa wabunge mahiri katika kambi ya upinzani ‘aliyenikosesha raha’ katika kiti cha uspika nilichokuwa nimekikalia. Kila mara alinitumia ki-‘memo’ kunikumbusha kuwa nikimwita jina lake, mwishoni nitaje ‘Mbunge wa Arumeru Mashariki’, ilhali akijua kuwa wabunge wote wa bunge lile kivuli hawakuwa na majimbo! Walikuwa ni wabunge wa kitaifa. Mbunge huyo hakuwa mwingine bali ni wewe Joshua Nassari.

Hiyo ilikuwa ni mwaka 2009. Tayari ulikuwa na ndoto za kuwania ubunge wa Arumeru Mashariki. Mara kadhaa ulinishawishi kuwa lazima vijana tushike nafasi za uongozi ili tulete mabadiliko. Niliposema kushika nafasi za kisiasa sio sawa na kumkomboa myonge, ulinikosoa: ‘Wewe ‘political scientist’ (mwanasayansi wa siasa) gani usiyependa siasa?’ Nami nikakutahadharisha kutofautisha kati ya siasa na madaraka huku nikimnukuu Prof. Shivji: ‘[M]imi si mwanasiasa, ingawa ninapenda siasa. Wanasiasa huwa hawapendi siasa, wanapenda madaraka‘. 

Kwa kuwa tulikuwa tukiishi mtaa mmoja, aghalabu tulikutana kwa mama ntiliye na kuanza kutaniana. ‘Mheshimiwa Spika, hata wewe unakula kwa mama ntiliye?’ Ila tukajifariji: sisi ndio wawakilishi halisi wa wanyonge. Tunapanda nao daladala na tunakula nao kwa mama ntiliye. Na hatukufanya hivyo kwa kuigiza bali ndivyo maisha yalivyotulazimisha.

Lakini sasa wewe si mbunge-kivuli tena. Ni mbunge wa ukweli. Hutalazimika kuazima koti na tai au kushangilia hotuba yako iliponukuliwa gazetini au sura yako kuonekana katika televisheni [kama tulivyokuwa tukifanya enzi zile]. Hivi sasa, ili magazeti yauze sharti yaandike habari zako, iwe za kweli ama za uongo. Nafasi yako inakurusha mbali kimaisha na watu waliokuchagua. Ukipanda daladala au kula kwa mama ntiliye, utafanya hivyo kwa kuigiza si kwa kulazimishwa na hali ya kipato chako. Mwisho wa mwezi huu, bila shaka, akaunti yako itakua na salio lisilopungua milioni kumi! Tena utaongezewa zingine milioni tisini kwa ajili ya gari. Hayo ndio maisha mapya ya uwakilishi wa wananchi. Sina hakika kama dhana ya uwakilishi inaleta maana hapa.


Ningependa kukukumbusha sehemu ya hotuba yako katika Bunge Kivuli mwaka 2009. Kila mmoja alikereketwa kwa utamu wa hotuba zako zenye mrengo wa kimapinduzi na zilizofanyiwa tafiti. Iwapo umepoteza mkanda wa Bunge lile, nitakusaidia kunukuu sehemu ya hotuba yako kuhusu nini kifanyike ili kuiokoa elimu yetu:
Mheshimiwa Spika, ukweli ni kwamba elimu yetu ni kivuli hafifu cha elimu ya kikoloni: imekosa ubora uliokuwa ndani ya elimu ya kikoloni ya wakati ule na pia imekosa maudhui ya kiukombozi kwa sababu haionekani kuwa na malengo thabiti yanayoangalia mustakabali wa nchi yetu. Katika vigoda hivi viwili, elimu yetu imedondoka sakafuni.
Mheshimiwa Spika, tumekataa kukubali kwamba mfumo mzima wa elimu yetu umevurugika baada ya kukubali kwamba turudi katika chumba cha usanifu na kuuchora mfumo huo upya. Tumehangaika kujenga vyumba vingi zaidi na kuelezea ujinga kwa gharama kubwa.
Mheshimiwa Spika, kinachohitajika katika mfumo wa elimu yetu si jambo jingine bali ni mapinduzi ya elimu ambayo yataandamana na elimu ya mapinduzi itakayozagaa katika sekta zote muhimu. Hii ni kwa sababu, tukatae tusikatae, sekta kadhaa muhimu nazo zina taswira ileile tunayoiona katika sekta ya elimu. Napenda kuchukua fursa hii kuangazia nini kifanyike ili kuhakikisha kuwa serikali inatoa elimu bora na si bora elimu. Katika hili, nisingependa kuwa nyuma kuunga mkono baadhi ya mitazamo ya wanafalsafa walioweza kuitoa kuhakikisha kuwa sekta ya elimu nchini inaboreshwa. Mitazamo hii ni pamoja na ifuatayo:-
*      Kuwatendea haki walio wengi ambao tunajua kuwa hawataingia katika vyuo vya elimu ya juu. Hali inaonyesha kuwa ni sehemu ndogo tu ya watoto wanaoingia shule za msingi ndio wanaopata nafasi ya kuendelea hadi Chuo Kikuu.  Tujenge mifumo ya elimu na mitaala itakayowafanya watoto wa nchi hii wawe na manufaa kwa jamii zao; watoto wa wakulima wafundishwe kilimo bora, watoto wa wafugaji wajifunze ufugaji bora, n.k.
*      Tuwekeze kwa dhati kwa kutenga rasilimali za kutosha na kuwekeza katika tafakuri ya pamoja katika shule za umma na kuzifanya ziwe na ubora wa hali ya juu kiasi kwamba isiwepo haja ya wazazi kuwapeleka watoto wao katika shule binafsi, ambazo ni za gharama kubwa zaidi.               
*      Shule ifundishe sayansi, hisabati na lugha. Lakini pia ifundishe maadili mema ili kujenga raia wema. Sayansi, teknolojia, hisabati na lugha ni nyenzo muhimu katika makuzi ya kijana. Lakini iwapo nyenzo hizo hazitaambatana na mafunzo na malezi ya uungwana ipo hatari watazitumia nyenzo hizo katika uhalifu.
*      Watoto wafundishwe na watiwe shime ya kufanya tafakuri ya kiudodosi (‘critical thinking’). Aidha, vijana wa Tanzania wafundishwe kujiamini, kutafakari na kusema kwa sauti kile wanachokiamini. Pamoja na maadili, watoto pia wafundishwe kupenda vitu vizuri ikiwa ni pamoja na umaridadi, michezo na sanaa ikiwa ni pamoja na muziki na ushairi kama sehemu ya ujenzi wa jamii ya watu wanaopenda mazingira wanayoishi maisha ya siha na furaha. Elimu inayomfunza mtoto hisabati lakini haimfundishi namna ya kuvaa vizuri, kula kwa staha na kuongea kwa ufasaha katika lugha anayoheshimu hadhira inaunda roboti na si binadamu.
*      Suala la ubora wa elimu ya walimu liwe nambari moja kwa sababu bila walimu bora, yote mengine tunayoyafanya, kama vile ujenzi wa majumba, n.k. ni upuuzi. Walimu watokane na wahitimu wenye ubora wa juu kuliko wengine, watambulike kwa uwezo wao mkubwa katika masomo yao, waandaliwe vema, walipwe mishahara mizuri na wapewe marupurupu wanayostahili…
Hebu itazame nukuu ya hotuba yako hapo juu. Hayo yalikuwa ni mawazo yako katika Bunge Kivuli miaka miwili iliyopita. Sina hakika ni wangapi hutoa mawazo ya aina hiyo katika Bunge uingialo ambalo ajenda yake kuu ni ‘mipasho na miposho’. Ulitaka tujitazame kama jamii, tusiangalie tulipoangukia bali tuchunguze tulipojikwaa. Ulisisitiza kuwa maendeleo hayapimwi kwa vitu bali ubora wa maisha ya watu. Ulitaka tufanye tafakuri ya kina kama jamii na kufikia mwafaka wa jamii tuitakayo. Ulisisitiza tufanye mabadiliko ya kimfumo yatakayojenga taasisi zenye kujali maslahi ya wengi.

Naamini utajinoa zaidi kinadharia ili usiwe mbwabwaja maneno kwa kuchukulia matatizo yanayozalishwa na mfumo wa kinyonyaji tulioukumbatia, kuwa mtaji wako wa kisiasa. Naamini utakinoa chama chako ili kijitaje kinadharia na kivitendo, je, umma kinaoupigania ni umma gani? Je, umma huo utakombolewa na itikadi/dira gani? Je, umma huo utakombolewa na nani? Je, ni miiko ipi inapaswa kutawala maisha ya viongozi na wanachama?

Ngoja nikutolee mfano: TANU na CCM ya mwalimu Nyerere ilichagua umma wa wanyonge [wakulima na wafanyakazi] huku itikadi yake ya ukombozi ikiwa Ujamaa. Pamoja na mapungufu kadhaa ya utekelezaji wa Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, wananchi wetu bado wanalikumbuka Azimio la Arusha na kusema: ‘Azimio lilitujali!’ Hata juzi machinga walipofukuzwa katika eneo la Ubungo, ambapo huuza bidhaa zao wakati wa jioni, waliimba: ‘Kama sio juhudi zako Nyerere, na amani ingetoka wapi?’ Wanatambua kwamba amani ni tunda la haki; amani hupatikana kwa kujenga mfumo unaojali maslahi ya wengi. Ndivyo alivyofanya Mwalimu.

CCM ya sasa pia ina umma wake –  wawekezaji-papa na wafadhili – na itikadi yake ni uliberali mambo-leo [soko huria]. Machinga, wakulima wadogo, wachimbaji wadogo, mama ntiliye n.k. sio umma wa CCM. Wao ni uchafu, sio injini ya maendeleo katika soko huria. Ndio maana hunyang’anywa ajira zao, hunyanyaswa na kusukumwasukumwa ovyo. Huporwa hata kile kidogo walicho nacho. Hivyo haishangazi, wakati wananchi wakilalamika kwa hali ngumu ya maisha,  watawala huwashangaa huku wakisema, ‘huko nje tunasifiwa’.

Najua unajiandaa na sherehe ya kuapishwa. Naomba nikugawie kipande cha keki niliyopewa na Prof. Shivji wakati nikihitimu shahada ya kwanza mwaka 2011. Ni keki isiyoisha, isiyooza, isiyopungua utamu:

Maisha sio porojo
Za siasa na Abunuwasi.
Maisha sio uhondo
Wa dhahabu na almasi
Maisha sio uhongo
Wa ufisadi na uchoyo
Wa mali na madaraka.
Maisha ni kuishi
Kuishi uhai wa walalahoi.

Maisha ni kujitolea
Mhanga wa ukombozi
Ukombozi wa kitabaka
Tabaka la wanyonywaji
Tabaka la wanyanyaswaji.
Nakutakia kila la heri katika utekelezaji wa majukumu yako.

Wasalaam,
Sabatho Nyamsenda,
Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Siasa,
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
6/4/2012.