25/04/2009

Wabongo wawakilisha vyema Dublin

Alhamisi ya wiki hii hapa University College Dublin (UCD), Ireland ilifanyika warsha iliyoambatana na uwasilishwaji wa mada zinazohusu utafiti katika nyanja ya maendeleo. Warsha hiyo iliyoandaliwa na Programme of Strategic Co-operation between Irish Aid and Higher Education and Research Institutes, ililenga kutambulisha kazi za kitafiti zinazofanywa na wanafunzi wa shahada ya uzamivu (PhD in Global Human Development). Nchi ya Ireland kupitia taasisi ya Irish Aid pamoja na Higher Education Authority inadhamini masomo ya jumla ya wabongo kumi kutoka University of Dar es Salaam, ikishirikiana na chuo hiki. Kwa ujumla wabongo hawa waliwakilisha vyema nchi yetu katika warsha hiyo na kwa kiasi kikubwa kuwaonesha  wazungu (siku hizi wanapenda kuitwa partners in development), kuwa si haba katika kutumia utafiti kama njia ya kutoa matokeo yatakayoongeza mchango wa elimu katika kutatua matatizo mbali mbali ya jamii. Waweza kujipatia angalau kwa uchache wake, taswira za siku hiyo ya warsha hapa chini;

Mdau Lupa Ramadhani kutoka bongo akisisitiza jambo alipokuwa akiwasilisha mada

Mdau Engineer George Lupakisyo Mwalwiba kutoka bongo akiwasilisha mada yake

Mmoja wa watoa mada, Michelle D'Arcy kutoka UCD.

Rais wa UCD, Dr. Hugh Brady akizungumza wakati wa warsha hiyo


Sehemu ya washiriki wa warsha hii, wakiwemo wanafunzi wa uzamili wakifuatilia uwasilishwaji wa mada

Baadhi ya washiriki katika warsha wakifuatilia

Mdau Herieth Rwezaura kutoka bongo akishusha nondo alipokuwa akiwasilisha mada

Mdau Joel Silas Kaswalalah kutoka bongo akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada yake

Huyu jamaa naye aliwasilisha mada

Mdau Luka Mkonongwa kutoka bongo akiwasilisha mada

Wenzetu nao hawakuwa nyuma, huyu jamaa anaitwa Morris Niall kutoka UCD, naye aliwasilisha mada




3 comments:

  1. nawashukuru hao wadau kwa kutuwakirisha inaletesha moyo na inapendeza kuona hawakuwa/hatupo nyuma.

    ReplyDelete
  2. Saaafi sana. Nina uhakika wako wengi na mahala pengi wakifanya mema mengi lakini hawaonwi na wengi.
    Asante kwa kuwaona, kuwatambua na kuwawakilishia kazi zao nzuri hapa
    Baraka kwenu

    ReplyDelete
  3. Mzee nimekubali, unajua tatizo ni kwamba si rahisi kujua nani yu wapi na anafanya nini. Nafikiri kwa jitihada kama hizi wengi tutawaona na kujua wanafanya nini na hatimaye kuhamasisha wengi ambao wanahitaji kutiwa moyo ili wafanye makubwa zaidi.Big up bro,na wengine toka nchi nyingine watuonyeshe pindi wanapoitoa bongo kimasomaso.

    ReplyDelete