Ni asubuhi nimeamka
Mwili unachemka
Kijasho kinaniteremka
Kwa ndoto niliyoota
Nilipopanda kitandani
Nilipotoka salani
Kichwa changu mchagoni
Nikapitiwa usingizi
Wala sikuhisi baridi
Na kujifunika zaidi
Hata sikusikia radi
Ndoto nikaanza 'ota
Naanza ingia chomboni
Na kuruka mawinguni
Chombo ni ndege jamani
Tupo juu sana angani
Tumeruka juu sana
Tena kwa kasi hapana
Tunakata wingu pana
Kwa raha na utulivu
Mara ghafla yatokea
Chombo chaanza potea
Chayumba na kulegea
Hatari wanatutangazia
Chini kwa kasi twashuka
Moyo unanishtuka
Huku macho yamenitoka
Nahisi roho kunitoka
Purukushani za angani
Zamalizikia baharini
Ndege yajikita majini
Pumzi kubwa naishusha
Punde tunaanza tolewa
Nje kuliko na hewa
Mizigo yetu tunapewa
Vingine ninapotelewa
Mara nauona mwanga
Wapiga kama upanga
Ninakaa na kujipanga
Ni ndoto ya Jumapili!
Mmmmh!
ReplyDelete